Moja kati ya ahadi alizitoa Rais wa Marekani Donald Trump akiwa kwenye kampeni zake ni pamoja na kuzuia wahamiaji kuingia nchini humo ambapo ripoti mpya zimesema Donald Trump atasaini sheria ya kuzuia kwa muda vibali vya wahamiaji kutoka Iran na nchi nyingine sita.
Taarifa za baadhi ya maafisa wa bunge la Marekani (Congress) na mtaalamu katika Idara ya Uhamiaji zimeeleza kwamba Rais Trump leo Jumatano anatarajia kusaini miswada kadhaa ikiwemo ya kusimamisha kwa muda utoaji visa kwa raia wa nchi za Kiarabu.

No comments:
Post a Comment