VYUO NA PROGRAMU ZILIVYOZUILIWA KUDAHILI WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA KWA MWAKA WA MASOMO 2017/18 - www.gbgraphixpro.com

Random Posts

test banner

Post Top Ad

Responsive Ads Here

VYUO NA PROGRAMU ZILIVYOZUILIWA KUDAHILI WANAFUNZI WA MWAKA WA KWANZA KWA MWAKA WA MASOMO 2017/18

Share This
upload_2017-7-24_22-40-20.png
1.0 Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inapenda kuuarifu umma kuwa, mwezi Septemba na Oktoba mwaka 2016 ilifanya uhakiki wa vyuo vyote vya elimu ya juu nchini ili kuhakiki ubora wa elimu inayotolewa vyuoni. Ripoti ya uhakiki ilionesha mapungufu kadhaa katika baadhi vyuo. Kwa sababu hiyo, Tume imesitisha udahili wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/18 kwa vyuo vifuatavyo:
  1. Eckenforde Tanga University
  2. Jomo Kenyatta University, Arusha
  3. Kenyatta University, Arusha
  4. United African University of Tanzania
  5. International Medical and Technological University (IMTU)
  6. University of Bagamoyo
  7. Francis University College of Health and Allied Sciences
  8. Archibishop James University College
  9. Archibishop Mihayo University College
  10. Cardinal Rugambwa Memorial University College
  11. Kampala International University Dsm College
  12. Marian University College
  13. Johns University of Tanzania Msalato Centre
  14. Johns University of Tanzania, Marks Centre
  15. Joseph University College of Engineering and Technology
  16. Teofilo Kisanji University
  17. Teofilo Kisanji University Tabora Centre
  18. Tumaini University, Mbeya Centre
  19. Kilimanjaro Christian Medical University College (KCMCo)
2.0 Aidha, kutokana na mapungufu katika vyuo mbalimbali imeamriwa kwamba jumla ya programu 75 kutoka vyuo 22 nchini zimesitishwa kudahili wanafunzi wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/18. Kuona Programu ambazo zimesitishwa kudahili wanafunzi kwa mwaka wa masomo 2017/18 tafadhali bonyeza hapa.

3.0 Aidha Tume inapenda kusisitiza kwamba, uamuzi huu hautawahusu wanafunzi wanaondelea na masomo katika programu na vyuo husika.

Imetolewa na:

Prof. Eleuther Mwageni

Kaimu Katibu Mtendaji

24 Julai 2017

No comments:

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages