
Hatimae serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya uchukuzi imesaini mkataba wa awamu ya kwanza ya ujenzi wa Reli ya kisasa itakayowezesha Treni zinazotumia umeme kuanza kufanya kazi kwa mara ya kwanza Tanzania.
Waziri wa uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amesema ‘Sasa hivi kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza unatumia saa 36 ambapo kuna kilometa 1219 lakini Treni mpya za umeme zikianza kufanya kazi safari itakua rahisi zaidi‘
‘Leo tunashuhudia utiaji saini makubaliano ya ujenzi wa sehemu ya kipande cha reli kati ya Dar es salaam na Morogoro chenye urefu wa kilometa 300 na mkataba huu utakua baina ya RAHACO kampuni hodhi ya rasilimali za reli na ubia kati ya kampuni ya UTURUKI na URENO’
No comments:
Post a Comment